Tuesday 7 January 2014

Kikao cha Kijiji, Mei 2013. Je matokeo niaje?

Mwaka jana kilifanyika kikao pale Kisatuni kuzungumzia suala la wageni kuvamia hifadhi ya kijiji ,sehemu za Pela hadi mtoni. Wageni hao waliuziwa mashamba au misitu hiyo na baadhi ya viongozi wa kijiji. Lakini kati yao hakukuwa na hata mmoja aliyekuwa na hati miliki ya ardhi. Viongozi wahusika waliingia mtini siku hiyo ya kikao.

Wanakijiji waliwakomalia wageni hao kuwa wavune mazao yao kisha waishie au watafute maeneo halali.
Je suala hili utekelezaji wake umefikia wapi? Wabwanga mbuli ino mwimanya, hegu?!!

Baadi ya picha siku ya kika hicho.


 Masudi Mbalazi akimwaga hoja zake.
 Juma Mgaza aliendesha kikao hicho.


 Mzee Mtiga akitoa hoja yake.


Mmoja wa wageni hao ajijitetea.

No comments:

Post a Comment